#Local News

MAHAKAMA YA NAIROBI IMEWAPA MAAFISA WA DCI SIKU NNE KUWASHIKILIA WASHUKIWA WAWILI WA DR VICTORIA

Mahakama ya Nairobi imewapa maafisa wa DCI siku nne zaidi kuwashikilia washukiwa wawili, Daniel Mwangi na Kevin Kinuthia, huku uchunguzi wa mauaji ya Dkt. Victoria Mutiso ukiendelea.

DCI ilikuwa imeomba siku saba zaidi ili kukamilisha uchunguzi, ikisema imepata taarifa mpya kutoka kwa washukiwa na watu wengine waliokamatwa.

Mahakama imesema washukiwa hao wazuiliwe kwa siku nne pekee, huku polisi wakisubiri ripoti za uchunguzi wa kisayansi na fedha, pamoja na kuwasaka mashahidi wengine.

Imetayarishwa na Jesca Angeyo

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *