#Rugby #Sports

KCB YAILAZA KABRAS KUTWAA TAJI LA EMBU 7S

KCB imeibuka mabingwa wa Embu 7s baada ya kuilaza mpinzani wake Kabras Sugar 7s kwa alama 12 kwa 10 katika fainali ya Kombe, na kutwaa taji katika awamu ya sita ya mzunguko wa kitaifa wa mwaka huu

Ushindi huo umeipa KCB nafasi nzuri zaidi katika msimamo wa jumla wa mfululizo, huku ikiwa ni mara ya tatu ndani ya awamu tano msimu huu kwa KCB na Kabras kukutana katika fainali ya Kombe

KCB imeendelea kutawala mikutano hiyo muhimu baada ya kuishinda Kabras tena, huku Embu 7s ikiwa ni awamu ya pili kutoka mwisho katika mzunguko wa National 7s Circuit wa 2026.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *