#Rugby #Sports

STRATHMORE LEOS YALENGA KUREJESHA TAJI LA EMBU SEVENS

Nahodha Gabriel Ayimba anaamini Strathmore Leos iko tayari kurejea kwa nguvu baada ya matokeo mabaya ya Driftwood Sevens, huku ikilenga kutwaa Embu Sevens kwa mara ya tano mfululizo.

Leos ilimaliza nafasi ya 14 Mombasa ikiwa na alama mbili pekee, lakini Ayimba amesema kikosi kimejifunza kutokana na makosa hayo na kinafanya maandalizi makali kurejea katika kiwango chake.

Strathmore imetawala Embu Sevens katika misimu minne iliyopita, ikiwahi kuwashinda Menengai Oilers, Catholic Monks na KCB, huku Ayimba akiamini rekodi hiyo inaweza kuendelezwa wikendi hii.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *