WAKENYA WALIO NCHI ZA NJEWAMEHIMIZWA KUFUATA SHERIA ZA KUINGIA NCHI HIZO
Wakenya wanaoishi katika nchi jirani wamehimizwa kufuata sheria na masharti ya kuingia katika nchi hizo, ili kudumisha ushirikiano mzuri katika Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Waziri Mkuu Musalia Mudavadi amesema Kenya inaheshimu ushirikiano na nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, na kuwataka Wakenya kuheshimu sheria za nchi hizo.
Kauli hiyo inajiri baada ya Rais William Ruto kuagiza wageni wanaofanya biashara ndogo ndogo nchini Kenya kuhakikisha wana hati na vibali vinavyohitajika.
Imetayarishwa na Jesca Angeyo
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































