#Local News

MOTO WATEKETEZA MADUKA SOUTH B, NAIROBI

Moto mkubwa umezuka katika maduka yaliyoko kando ya Barabara ya Kapiti eneo la South B jijini Nairobi, huku ripoti zikisema moto huo umeanea hadi makazi ya Golden Gate Estate.
Moto huo ulianza mwendo wa saa sita usiku wa kuamkia Jumatatu na kuendelea hadi saa za mapema asubuhi, huku video zikionyesha moshi mzito na miali mikubwa ikipanda kutoka kwenye majengo ya eneo hilo.
Chanzo cha moto huo pamoja na ukubwa wa hasara bado hakijafahamika, huku juhudi za kudhibiti moto huo zikiendelea.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *