#Sports #Volleyball

MALKIA STRIKERS YAKATA TIKITI YA NUSU FAINALI

Malkia Strikers imefuzu nusu fainali ya Mashindano ya Afrika ya Mpira wa Wavu kwa Wanawake baada ya kuichapa Algeria kwa seti 3-1 katika robo fainali iliyochezwa Kasarani.

Algeria ilianza kwa kishindo na kushinda seti ya kwanza kwa alama 25-21, lakini Malkia Strikers ilirejea kwa nguvu mbele ya mashabiki wa nyumbani na kushinda seti tatu zilizofuata.

Mabingwa hao watetezi sasa watakutana na Cameroon katika nusu fainali Alhamisi, baada ya Cameroon kuichapa Uganda kwa seti 3-0 na kutinga hatua hiyo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *