KCB YAKOSA NYOTA WATANO KUELEKEA CHRISTIE SEVENS
KCB RFC itaingia katika hatua ya mwisho Ubingwa wa Kitaifa na Mahindano ya Christie Sevens jijini Nairobi wikendi hii bila nyota wake watano muhimu.
Nahodha Vincent Onyala, George Oroo, Festus Shiasi, Nigel Amaitsa na Samuel Asati wataelekea Wales kushiriki michuano ya kwanza ya Ultimate Sevens Championship jijini Cardiff Jumamosi.
Hata hivyo, kocha Andrew Amonde anapata nafasi ya kuwapa wachezaji wa kikosi cha pili majukumu makubwa katika harakati za KCB kutetea ubingwa wa Christie Sevens na National Sevens Circuit.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































