#Football #Sports

KARIOBANGI SHARKS YAKABILIWA NA FKF KWA KUPINGA KUSHUSHWA DARAJA

FKF imeiita Kariobangi Sharks mbele ya Kamati ya Nidhamu kwa madai ya kuidhalilisha soka baada ya klabu hiyo kupeleka kesi yake ya kushushwa daraja katika Mahakama Kuu.

FKF inadai Sharks ilikiuka sheria za ndani, za bara na za FIFA kwa kutumia mahakama ya kawaida kupinga kushushwa kwake kutoka ligi kuu, baada ya kumaliza nafasi ya 16 msimu wa 2025/26.

Sharks inasisitiza kuwa kanuni za 2019 ndizo zilipaswa kutumika na hivyo kupewa nafasi ya mchujo wa kushuka daraja, huku FKF ikisema kanuni hizo zilibadilishwa kabla ya msimu kuanza.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *