#Local News

IEBC YAONYA JUU YA KUONGEZEKA KWA VURUGU ZA UCHAGUZI

Wadau wa uchaguzi wameonya kuhusu kuongezeka kwa visa vya vurugu za kisiasa katika maeneo mbalimbali nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa 2027, wakisema hali hiyo inatia wasiwasi.

Katika mkutano wa usalama na IEBC jijini Nairobi, wadau wametaja Homa Bay, Nakuru, Bomet na Migori, wakisema mwenendo huo unafanana na hali iliyotangulia ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007 na 2008.

Mwenyekiti wa IEBC Erastus Ethekon amesema takriban maafisa 200,000 wa polisi wanaendelea na mafunzo kuelekea uchaguzi huo, katika juhudi za kuimarisha usalama na amani.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *