MISHENI YA HAITI YAPATA PIGO, TENA

Mpango wa kenya kuwatuma maafisa wa polisi nchini Haiti umepata pigo kwa mara nyingine, baada ya wakili Ekuru Aukot kuelekea mahakamani akitaka mahakama kusimamisha mpango huo, akisema serikali imekiuka agizo la mahakama la Jaunuari kusitisha mpango huo.
Katika ombi lake, anasema serikali tayari imewachagua maafisa 200 wa polisi ambao wameratibiwa kuondoka mwishoni mwa wiki hii.
Aidha, amesema serikali inakiuka sheria maksudi kwa kuendelea na alichokitaja kuwa ni shughuli haramu ya kuwatuma polisi Haiti.
Imetayarishwa na: Antony Nyongesa
English 





































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































