TUKO PABAYA KIFEDHA, SRC
Mwenyekiti wa tume ya kuratibu mishahara ya wafanyakazi wa umma SRC Lynn Mengich ameibua hofu kuhusiana na kiwango cha juu cha fedha zinazotumiwa katika kulipa mishahara, ambacho kwa sasa ni asilimia 43 ya mapato ya serikali.
Akizungumza na wanahabari, Mengich amesema matumizi ya fedha za serikali yamekuwa yakiongezeka licha ya juhudi za serikali kubana matumizi.
Aidha, amesema matumizi hayo ambayo yamezidi shilingi trilioni moja, pia yamezidi kiwango cha asilimia 35 kinyume na sheria za usimamizi wa fedha za umma.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 







































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































