KENYA, UHOLANZI ZASHIRIKIANA
Setkta ya kilimo nchini inatarajiwa kuimarika kufuatia udhabiti wa ushirikiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na Uholanzi, mataifa hayo mawili yakitia Saini mikataba kadhaa ya ushirikiano ikiwemo kilimo.
Kutiwa Saini kwa mikataba hiyo kumewekwa wazi na Rais William Ruto katika Ikulu ya Nairobi ambako mfalme wa Uholanzi Willem Alexander na mkewe Malikia Maxima wamepokelewa.
Kwa upande wake, mfame huyo ambaye yuko ziarani nchini, amepongeza uhusiano wa kidiplomasia kati ya Kenya na taifa lake ambao umedumu kwa miaka Zaidi ya miongo 6.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































