#Local News

HOFU YA AJALI BARABARANI

Hofu imeibuka nchini kuhusu ajali za barabarani, zaidi ya watu 20 wakiaga dunia kwenye ajali hizo katika kipindi cha siku 5 za mwanzo wa mwaka huu pekee huku wito ukitolewa kwa madereva kuwa makini.

Hii ni baada ya watu 9 kufariki kwenye ajali katika eneo la Naivasha hapo jana na wengine 55 kujeruhiwa, ajali ambayo imehusishwa na uchovu wa dereva mbali na kuhudumu kwa saa nyingi bila kupumzika.

Waziri wa uchukuzi Davis Chirchir, na kamanda wa polisi eneo la Naivasha Wilson Sigei, wamewataka madereva kuchukua tahadhari.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

HOFU YA AJALI BARABARANI

AMOLLO: HATUJAPANGA KUMTIMUA SIFUNA

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *