#Local News

FAMILIA YA JEFF MWATHI YAOMBA MAHAKAMA KUHARAKISHA KESI


Familia ya Jeff Mwathi imeomba mahakama ziendelee haraka na kwa ufanisi na kesi inayohusu kifo chake, ikieleza kuwa mchakato huo umekuwa wa kusababisha maumivu makubwa kwao.

Kupitia wakili wao, Danstan Omari, familia imebainisha kuwa Mwathi alizikwa mara mbili, jambo lililozidisha huzuni yao na kuendelea kuendeleza maumivu ya kifamilia.

Familia imetaja kuwa wako tayari kujitokeza mahakamani wakati wowote kuhakikisha kesi inasikilizwa na kufikiwa uamuzi bila ucheleweshaji wakitafuta haki na amani ya moyo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *