#Football #Sports

KAKAMEGA HOMEBOYZ YAOMBOLEZA MLINZI SILAS ABUNGANA

Kakamega Homeboyz FC na familia ya soka nchini Kenya wamegubikwa na mshtuko kufuatia kifo cha ghafla cha mlinzi wao, Silas Abungana.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, aliyekuwa amejiunga na klabu hiyo kutoka Shabana mwanzoni mwa msimu huu, alidaiwa kushambuliwa na ndugu yake mdogo katika mzozo mkali kuhusu kipande cha ardhi ya familia.

Mchezaji huyo aliaga katika Hospitali ya Kaunti ya Kakamega alifariki kutokana na majeraha aliyoyapata.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *