SERIKALI INACHUNGUZA ‘MGENI’ ALIYEWAHADAA WANAWAKE
Hofu imeibuka kuhusiana na usalama wa wanawake nchini kutokana na ripoti ya raia mmoja wa kigeni kudaiwa kuwahadaa wanawake kadhaa na kuwapeleka katika makazi yake nchini, akarekodi na kusambaza picha za siri za wanawake hao bila idhini yao wala ufahamu wa idara ya ujasusi.
Kulingana na msemaji wa serikali Isaac Mwaura, idara ya usalama, upelelezi na ile ya mashtaka zimeagizwa kuchukua hatua Madhubuti kwa ushirikiano na mamlaka za kimataifa, ikizingatiwa kuwa mshukiwa ni raia wa kigeni.
Amewahimiza wakenya kudumisha maadili yao.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































