KNH YATOA NOTISI KUHUSU MIILI ISIYODAIWA
Hospitali ya Kitaifa ya Kenyatta imetoa tangazo kwa umma ikizitaka familia kudai miili 480 iliyopo katika hifadhi yake, ikionya kuwa itazikwa ndani ya siku saba iwapo haitatambuliwa.
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa hii leo, miili hiyo inajumuisha watu wazima 102 na watoto 378, jambo linaloonyesha uzito wa hali hiyo.
Uongozi wa hospitali hiyo umetoa wito kwa jamaa na walezi kujitokeza haraka kutambua na kuchukua miili hiyo ili kuepusha hatua ya kuizika kwa mujibu wa sheria.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 

















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































