#Football #Sports

RASHFORD AWAPA BARCA UBINGWA LA LIGA

Bao la ikabu la Marcus Rashford liliwawezesha Barcelona kuwalaza mahasimu wao Real Madrid kwa kichapo cha mabao 2-0 katika mechi ya La Liga na kutawazwa mabingwa zikiwa zimesalia mechi 3 kabla ya ligi hiyo kutamatika.

Mshambulizi huyo wa Uingereza aliwaweka Barcelona kifua mbele kabla ya Ferran Torres kufunga la pili kuwapa miamba hao ushindi katika debi ya El Classico ugani Nou Camp.

Kwa sasa Barca wako mataji 7 nyuma ya Real ambao wanashikilia ubingwa huo mara nyingi, ila Barca wameshinda taji hilo kwa misimu miwili mtawalia.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *