#Football #Sports

MATHARE UNITED YATANGAZA KUONDOKA KWA KOCHA JOHN KAMAU

Mathare United imetangaza kuondoka kwa kocha mkuu John Kamau huku mechi tatu pekee zikisalia kabla ya kumalizika kwa msimu wa Ligi Kuu ya FKF 2025/2026.

Klabu hiyo imesema Kamau ataondoka mara moja kutoka nafasi yake ya ukocha huku Kocha msaidizi Mohammed Mchulla akipewa jukumu la kuiongoza timu hiyo kwa muda katika mechi zilizobaki za msimu huu.

Hatua hiyo imefuatia kipigo cha mabao 2-0 dhidi ya APS Bomet, matokeo yaliyoripotiwa kuwa sababu kuu ya uamuzi huo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *