AFYA YA UMMA NAIROBI YATAHADHARISHA MGOMO
Maafisa wa afya ya umma jijini Nairobi wameituhumu bodi ya huduma ya kaunti kwa kuajiri maafisa wasio na sifa kushughulikia usalama wa chakula na uthibitisho wa afya.
Kupitia Chama cha Maafisa wa Afya ya Mazingira na Afya ya Umma, Katibu Mkuu wa chama Brown Ashira amesema hatua hiyo inakiuka sheria za afya ya umma na kanuni za usimamizi wa wataalamu wa afya.
Chama hicho kimeonya kuwa udhaifu katika usimamizi unaweza kuhatarisha usalama wa chakula na maji jijini, hali inayoweza kusababisha milipuko ya magonjwa ya kuambukiza.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































