KANZE DENA ADAI KUTISHWA NA SERIKALI
Msemaji wa afisi ya Rais wa nne wa Kenya Kanze Dena, amedai kwamba wafanyakazi katika afisi hiyo ambayo ni ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta wanapokea vitisho.
Akiwahutubia wanahabari, Dena aidha amedai kwamba serikali imedinda kuwapa kandarasi mpya wafanyakazi wawili kwenye afisi hiyo, ambao ni msimamizi wa afisi George Kariuki na mkurugenzi wa mawasiliano Kanze Dena Mararo.
Huku akionekana kupinga madai ya msemaji wa serikali Isaac Maura, Dena amesema serikali haijakuwa ikiyarekebisha magari wala kuwapa mafuta.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 






































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































