HAKUNA WIZI WA MTIHANI, WIZARA YAKANA
Huku uadilifu wa mtihani wa kitaifa wa kidato cha 4 KCSE ukitiliwa shaka kutokana na visa vya udanganyifu, serikali imesema kwamba mtihani huo uko salama kwamba hakujakuwa na udanganyifu wowote.
Akizungumza kwenye kaunti ya Meru mapema leo, katibu katika wizara ya elimu Dakta Belio Kipsang amesema majaribio ya wizi yamezimwa huku akiongeza kuwa karatasi za mtihani ambazo zimekuwa zikisambazwa mitandaoni ni ghushi.
Aidha Kipsang ametoa hakikisho kwamba masomo ya gredi ya 9 yanayoanza Januari yataendelea bila tashwishwi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































