#Local News

SIGEI ALAANI VURUGU KATIKA MIKUTANO YA KISIASA

Seneta wa Bomet Hillary Sigei amelaani vurugu na ukosefu wa uvumilivu katika mikutano na mikusanyiko ya kisiasa, akisema vitendo hivyo vinapaswa kukataliwa na kila Mkenya.

Sigei amesema hata wale ambao hawaungi mkono vyama vinavyohusika wanapaswa kulaani vurugu, akisisitiza umuhimu wa kuheshimu haki za kisiasa za wengine.

Kauli hiyo inajiri huku Kenya ikielekea katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2027, ambapo Sigei ametoa wito wa siasa za amani na uvumilivu ili kulinda mshikamano wa taifa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *