#Local News

NPS IMEANZA KUTAMBUA MAENEO YANAYOWEZA KUKUMBWA NA GHASIA IFIKIAPO UCHAGUZI MKUU

Huduma ya Polisi nchini, NPS, imeanza kutambua maeneo yanayoweza kukumbwa na ghasia za kisiasa kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2027.

Naibu Inspekta Jenerali wa Polisi, Gilbert Masengeli, amesema polisi watatumia taarifa za kiujasusi kutambua maeneo hayo na kuweka mikakati ya kuzuia vurugu.

Masengeli amesema polisi watahakikisha usalama wa wananchi unalindwa, huku akionya kuwa ghasia za kisiasa zinazochochewa na watu au makundi hazitakubaliwa nchini.

Imetayarishwa na Jesca Angeyo

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *