RUTO: MAENDELEO NI WAJIBU WA KIKATIBA WA SERIKALI
Katiba ya Kenya haijaweka msingi wa uongozi wa kidemokrasia pekee, bali pia inalenga kujenga taifa lenye ustawi wa kiuchumi na maisha bora kwa wananchi.
Rais William Ruto amesema Katiba ya Kenya inataka serikali kulinda demokrasia, kupanua fursa za maendeleo, kuimarisha utu wa binadamu na kuboresha maisha ya wananchi.
Ruto amesema maendeleo ni wajibu wa kikatiba wa serikali, akisisitiza kuwa mamlaka ya dola yanapaswa kutumika kuleta ustawi na kuongeza fursa kwa wananchi wote.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 



























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































