#Local News

HASSAN OMAR AJITETEA KUHUSU KAULI YA KURA ZA WAFU

Katibu Mkuu wa UDA Hassan Omar sasa amesema kauli yake kuhusu kura za wapiga kura waliofariki ilichukuliwa nje ya muktadha, akisema lengo lake lilikuwa kuwahamasisha Wakenya kujisajili na kushiriki uchaguzi mkuu wa mwaka ujao.

Omar amewashutumu viongozi wa upinzani kwa kupotosha matamshi yake na kupanga kuyatumia kudhalilisha chama tawala kwa manufaa ya kisiasa, akisisitiza kuwa hakulenga kuhalalisha matumizi ya kura za wafu.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *