KENYA IMEELEZEA DHAMIRA YAKE YA KUZINGATIA USALAMA WA NYUKLIA
Kenya imeeleza dhamira yake ya kuzingatia usalama wa nyuklia, huku serikali ikijiandaa kujenga kiwanda cha kwanza cha nguvu za nyuklia katika Kaunti ya Siaya.
Waziri wa Afya Aden Duale amesema Kenya imepiga hatua katika maandalizi ya mradi huo wa thamani ya shilingi bilioni mia tano. Alizungumza hayo katika mkutano wa IAEA mjini Vienna, Austria.
Duale amesema ujenzi wa kiwanda hicho unatarajiwa kuanza mwaka 2027, huku kikitarajiwa kuunganishwa na gridi ya taifa ifikapo mwaka 2034.
Imetayarishwa na Jesca Angeyo
English 












































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































