#Athletics #Sports

KENYA YAKOSA MEDALI MBIO ZA MITA 5,000 KWA WANAWAKE

Mbio za masafa marefu zinaendelea kuwa changamoto kwa Kenya katika Michezo ya Jumuiya ya Madola inayoendelea mjini Glasgow, huku wanariadha wake wakikosa nafasi ya kutwaa medali nyingine.

Wanariadha wa Kenya walikosa medali katika fainali ya mbio za wanawake za mita 5,000, huku Caroline Nyaga akimaliza katika nafasi ya tano kwa muda bora wa msimu wa dakika 14:54.00.

Rebecca Mwangi alimaliza katika nafasi ya 18, huku Rose Davies wa Australia akitwaa medali ya dhahabu kwa kutumia dakika 14:44.53, ikiwa ni dhahabu yake ya pili katika michezo hiyo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *