#Athletics #Sports

WAKENYA WAWIKA BERLIN

Wakenya walitangaza umahiri wao jijini Berlin kwenye mbio za Half Marathon, kutokana na kasi yao ya kuridhisha kwenye mbio hapo jana.

Andrea Kiptoo alimaliza wa kwanza katika mbio za wanaume kwa muda wa dakika 59:11, sekunde 3 pekee mbele ya mkenya mwenzake Dennis Kipkemoi, huku Mjerumani Amanal Petros akifunga nafasi tatu bora.

Katika mbio za wanawake, Likina Amebaw wa Ethiopia alimaliza wa kwanza katika muda wa 1:05.07, Ethiopia ikitawala nafasi 3 za kwanza.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *