#Local News

UPINZANI WAKATAA KUITWA WAASI, WAAHIDI KUIWAJIBISHA SERIKALI

Viongozi wa upinzani wamepuuza madai kwamba siasa za upinzani ni sawa na uasi, wakisisitiza kuwa jukumu lao ni kuikosoa na kuichunguza serikali kwa maslahi ya wananchi.

Viongozi hao wamesema wataendelea kuibua masuala yanayowahusu wananchi na kuitaka serikali kuwajibika kuhusu maamuzi na utekelezaji wa sera mbalimbali.

Wamesisitiza kuwa uwepo wa upinzani ni sehemu ya mfumo wa kidemokrasia, huku wakiahidi kutumia nafasi yao kufuatilia utendaji wa serikali na kuwasilisha hoja za wananchi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *