#Local News

MGOGORO WA UONGOZI WAZIDI KUIYUMBUA LINDA MWANANCHI

Mvutano wa kisiasa unazidi kuigawanya kambi ya Linda Mwananchi huku baadhi ya wanachama wakiegemea vyama tofauti wanapojiandaa kwa uchaguzi mkuu wa 2027.

Mbunge wa Embakasi Mashariki na anayewania ugavana wa Nairobi Babu Owino amesema kuna mvutano unaozidi kushika kasi ndani ya kambi hiyo.

Owino amesema anaunga mkono Seneta wa Nairobi Edwin Sifuna kuwania urais, lakini ameeleza kuwa atahudhuria baadhi tu ya mikutano ya Linda Mwananchi huku akisisitiza kuwa kambi hiyo inahitaji kuelewana kuhusu mwelekeo wake wa kisiasa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *