#Football #Sports

ULINZI STARS YALENGA KUANZA LIGI KWA KISHINDO DHIDI YA TUSKER

Kocha wa Ulinzi Stars Mulinge Ndeto anataka kikosi chake kipya kuanza msimu wa 2026/27 wa Ligi Kuu ya SportPesa kwa ushindi kitakapowakaribisha Tusker katika Uwanja wa Ulinzi Sports Complex Jumamosi.

Baada ya kunusurika kushuka daraja msimu uliopita, Ulinzi Stars imefanya mabadiliko makubwa katika kikosi huku Ndeto akisisitiza umuhimu wa kuongeza kasi na ubunifu katika safu ya ushambuliaji.

Ndeto anataka timu hiyo idumishe nidhamu yake ya jadi ya ulinzi huku ikiwa na makali zaidi mbele ya lango, mtihani ambao utaanza mara moja dhidi ya Tusker iliyoingia msimu ikiwa tayari kwa mashindano.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *