#Football #Sports

KOCHA WA TUSKER AKIRI UBINGWA UMEWAPONYOKA

Kocha mpya wa Tusker FC, Julien Mette, amekiri kuwa timu hiyo haina tena nafasi ya kuwania ubingwa wa Ligi Kuu ya SportPesa msimu huu.

Mette amesema sasa wataelekeza juhudi katika kuhakikisha wanamaliza katika nafasi tatu za juu kwenye msimamo wa ligi, pamoja na kuwania kombe la mashindano ya ndani.

Licha ya kupoteza kwa bao 1-0 dhidi ya Shabana FC katika Uwanja wa Gusii, kocha huyo amewasifu wachezaji wake kwa kiwango kizuri walichoonyesha. Bao la Thomas Teka liliipa Shabana alama zote tatu katika mechi hiyo iliyokuwa na ushindani mkali.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *