#Local News

RIGATHI ASHTUMU DCI KWA KUFICHA USHAHIDI DHIDI YA KIFO CHA VICTORIA MUTISO

Aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua amemshutumu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai DCI Mohamed Amin kwa kuficha madai ya kuhusika kwa polisi katika mauaji ya Victoria Mutiso.

Gachagua amedai kuwa kuna maswali ambayo hayajajibiwa kuhusu nafasi ya maafisa wa polisi katika kifo cha Mutiso akisisitiza kuwa mamlaka husika zinapaswa kuwajibika na kuhakikisha ukweli wote kuhusu tukio hilo unajulikana.

Kauli ya Gachagua inajiri huku uchunguzi kuhusu kifo cha Victoria Mutiso ukiendelea.

Imetayarishwa na Jesca Angeyo

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *