#Local News

NCIC YAMUITA KALUMA KUHUSU KAULI ZA KISIASA

Tume ya Kitaifa ya Uwiano na Utangamano, NCIC, imemwita Mbunge wa Homa Bay Mjini, Peter Kaluma, kufika mbele yake kuhusu kauli za kisiasa anazodaiwa kutoa katika Kaunti ya Homa Bay kabla ya mkutano wa Linda Mwananchi.

Kaluma ametakiwa kufika katika afisi za NCIC hapo kesho mwendo wa saa nne asubuhi, ili kusaidia katika uchunguzi unaohusiana na kauli anazodaiwa kutoa Agosti 15 mwaka huu.

Mwito huo umetolewa chini ya Sheria ya Kitaifa ya Uwiano na Utangamano, huku Kaluma akitarajiwa kutoa maelezo yake kwa tume hiyo kuhusiana na tuhuma zinazomkabili.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

NCIC YAMUITA KALUMA KUHUSU KAULI ZA KISIASA

NDINDI NYORO AJIUNGA NA UPINZANI

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *