#Football #Sports

HOMEBOYZ YAONYESHA IMANI KWA KOCHA EDWARD MANOAH

Meneja wa Kakamega Homeboyz Boniface Imbenzi amemuunga mkono kocha mpya Edward Manoah kuiongoza timu hiyo kufanya vizuri katika msimu mpya wa Ligi Kuu ya Kenya.

Imbenzi amesema uteuzi wa Manoah unalenga kubadili matokeo yasiyoridhisha ya misimu iliyopita, huku kocha huyo akisaidiwa na Paul Okatwa mwenye uzoefu wa kufanya kazi katika klabu hiyo hapo awali.

Amesema Okatwa amewahi kufanya kazi pamoja na makocha Francis Baraza na Patrick Odhiambo, jambo analoamini litasaidia benchi jipya la ufundi kuimarisha kikosi na kurejesha Homeboyz katika ushindani wa juu.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *