SERIKALI KUAGIZA MAGUNIA MILIONI 25 YA MAHINDI NCHINI
Serikali imetangaza mpango wa kuagiza magunia milioni 25 ya mahindi, kila moja likiwa na uzito wa kilo 90, ili kukabiliana na upungufu wa chakula unaoweza kusababishwa na ukame na athari za mabadiliko ya tabianchi
Waziri wa Kilimo Mutahi Kagwe amesema serikali tayari imeweka mipango ya kuwezesha uagizaji wa mahindi hayo, huku akiwahakikishia Wakenya kuwa hatua madhubuti zimechukuliwa kuhakikisha hakuna uhaba wa chakula nchini
Kagwe amesema uagizaji huo unalenga kuongeza akiba ya mahindi nchini na kuziba pengo linaloweza kujitokeza kutokana na kupungua kwa uzalishaji wa chakula kufuatia ukame na changamoto za hali ya hewa.
Imetayarishwa na Hilda Ajema
English 











































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































