#Local News

NDINDI NYORO AMTAKA RUTO KUACHA KUMSHAMBULIA UHURU

Mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro amemjibu Rais William Ruto kuhusu kauli zake za mara kwa mara dhidi ya Rais mstaafu Uhuru Kenyatta, akimtaka rais kuangazia changamoto zinazowakabili Wakenya badala ya kuendelea kurejea masuala ya zamani.

Nyoro amesema Ruto hashindani na Uhuru bali anakabiliana na hali ya kiuchumi inayowakabili Wakenya, akidai ugumu wa maisha umeongezeka chini ya utawala wa sasa..

Nyoro pia amesema iwapo Ruto anatarajia kuheshimiwa atakapoondoka madarakani, anapaswa kwanza kumheshimu Uhuru akiwa bado rais, huku akimtaka kuangazia masuala yanayowahusu wananchi.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *