#Local News

JUNET ADAI WABUNGE WALIHONGWA KUMNG’OA GACHAGUA

Mbunge wa Suna Mashariki, Junet Mohammed, amedai kuwa wabunge walipokea pesa kabla ya kupiga kura ya kumng’oa aliyekuwa Naibu Rais Rigathi Gachagua madarakani mwezi Oktoba 2024.

Akizungumza katika mkutano wa pamoja wa vyama vya UDA na ODM uliofanyika Kakamega, Junet alidai kuwa fedha zilitolewa kwa baadhi ya wabunge wa Bunge la Kitaifa na Seneti kabla ya kupitishwa kwa hoja ya kumwondoa Gachagua.

Aidha, Junet alidai kuwa baadhi ya wabunge hawakutumia pesa hizo ipasavyo, akiwashauri kujenga nyumba bora badala ya kuzitumia kwa mambo mengine.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *