#Local News

SERIKALI YAJIPANGA KUKABILIANA NA EL NIÑO

Wakati utabiri wa hali ya Hewa ukionyesha dalili za mvua kubwa ya El Nino, Waziri wa Utumishi wa Umma Geoffrey Ruku, amesema kuna uwezekano wa asilimia 80 wa nchi kushuhudia mvua za El Niño kati ya mwezi Oktoba na Desemba mwaka huu.

Ruku amesema serikali imeunda kamati maalumu inayoongozwa na Naibu Rais Kithure Kindiki ili kuratibu maandalizi ya kitaifa kabla ya kuanza kwa mvua hizo.

Aidha, amesema maandalizi hayo yanalenga kupunguza athari zinazoweza kusababishwa na El Niño na kuhakikisha nchi iko tayari kukabiliana na hali hiyo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *